JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

MAMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA

TAASISI YENYE VIWANGO VYA ISO 9001: 2015
Bw. Khalfan S. Saleh
Bw. Khalfan S. Saleh
Makamu Mwenyekiti

Bw. Khalfan S. Saleh ni Mtumishi wa Serikali katika Ofisi ya Rais. Ana Shahada ya Uzamili katika fani ya Mitandao ya Mawasiliano ya Kielekroniki (MSc Data Telecommunication Networks) kutoka Chuo Kikuu cha Salford, Uingereza. Amekuwa Serikalini kwa zaidi ya miaka 25 ambapo amepata fursa ya kufanyakazi katika Serikali zote mbili, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) pamoja na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (SMT). Nafasi alizowahi kushika ni pamoja na Balozi Mdogo katika Ubalozi wa Tanzania nchini Kenya, Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala wa Serikali wa Uchapaji Zanzibar na Mpigachapa Mkuu wa Serikali na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ.

Je, una Maswali yoyote juu ya Sekta ya Mawasiliano?
Tuma Mrejesho na Malalamiko!

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imejidhatiti kutoa huduma bora kwa wateja na wadau wake wote.

Tuma Mrejesho na Malalamiko!