Ujumbe wa Mkurugenzi Mkuu
Dkt. Jabiri Kuwe Bakari
Mkurugenzi MkuuKwa wadau wetu wapendwa!
Katika juhudi ya kufanikisha dira yetu ya kuwa: “Msimamizi wa Kiwango cha Kimataifa kwa Mawasiliano ya Elektroniki na Posta”, Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) inalenga kuimarisha uwezo wake wa kuhimiza ufikiaji wa huduma za mawasiliano na bidhaa kwa kila mtu kwa kushughulikia kimkakati mazingira ya usimamizi wa mawasiliano ya elektroniki na Posta yanayobadilika kwa kasi.
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) inalenga kujenga mazingira ya usimamizi yanayokuza uchumi wa kidigitali yanayochochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii nchini Tanzania.
Kutokana na mafanikio ambayo sekta ya mawasiliano imeyapata mpaka sasa, ni wajibu wetu kuhakikisha kuwa ujumuishaji wa teknolojia ya kidigitali hauna budi kuwafikisha wananchi wengi kwenye mawasiliano ya kimtandao katika Mkongo wa Taifa.
Miongoni mwa mambo mengine ambayo TCRA inakusudia kuyafanya ni kudumisha mazingira yenye ushindani na yanayofaa kwa uwekezaji wa sekta binafsi, kuwezesha upanuzi wa mtandao na huduma, matangazo kwa njia ya vyombo vya habari pamoja na utengenezaji wa maudhui ya ndani ya nchi, aidha TCRA itaendelea kuboresha miundombinu muhimu ya huduma za Posta na vifurushi kwa huduma za elektroniki na mifumo tumizi.
Ili kutimiza Dhamira yetu, TCRA itaendelea kuimarisha uelewa wa mtumiaji kwa njia mbalimbali za uelimishaji ili kuwaongezea na sikubainisha haki zao na majukumu tu bali pia kuwawezesha kufanya uamuzi arifu wakati wanapochagua huduma na bidhaa za mawasiliano.
Fauka na hayo, TCRA itaendelea kuimarisha uelewa wa watumishi wake kwa kuhakikisha kuwa wana afya na weledi ili watekeleze kwa kiwango cha juu cha uadilifu na uwajibikaji wakati wanapofanya shughuli za Mamlaka.
Mwisho, TCRA inaendelea na Dhamira yake ya kutoa huduma bora za usimamizi wa sheria si peke yao bali kwa kuzingatia “usimamizi kwa kushauriana” kama njia ya kuunda na kutekeleza muundo wa usimamizi bora na wenye tija.
Nawatakia mafanikio mema,
MKURUGENZI MKUU.