JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

MAMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA

TAASISI YENYE VIWANGO VYA ISO 9001: 2015

USULI NA HISTORIA

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ni taasisi iliyoasisiwa kwa mujibu wa sheria yenye wajibu wa kudhibiti sekta ya mawasiliano ya Kielektroni na Posta Tanzania. Ilianzishwa kwa Sheria ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) namba 12 ya mwaka 2003, ambayo iliunganisha zilizokuwa Tume ya Mawasiliano Tanzania (TCC) na Tume ya Utangazaji Tanzania (TBC).

TCC ilianzishwa 1993 na kupewa nguvu za kisheria kusimamia huduma za mawasiliano ya simu na Posta. Tume ya Utangazaji Tanzania (TBC) pia ilianzishwa 1993 na kupewa nguvu za kisheria kusimamia sekta ya utangazaji.

Kutokana na maendeleo ya teknolojia, umuhimu wa kuleta ufanisi kwenye utoaji wa huduma za Serikali kwa umma na kupunguza ukiritimba, kulikuwa na umuhimu wa kuunganisha tume mbili za usimamizi, TCC na TBC  na kuunda Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) mwaka 2003.

Mamlaka ilianza shughuli zake tarehe 1 Novemba 2003 ikichukua majukumu ya tume mbili zilizounganishwa. Majukumu ya TCRA yameainishwa kwenye Sheria ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania ya mwaka 2003, Kifungu cha 4 (1) hadi (7).

Je, una Maswali yoyote juu ya Sekta ya Mawasiliano?
Tuma Mrejesho na Malalamiko!

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imejidhatiti kutoa huduma bora kwa wateja na wadau wake wote.

Tuma Mrejesho na Malalamiko!