JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

MAMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA

TAASISI YENYE VIWANGO VYA ISO 9001: 2015

TCRA Kushiriki Kikao Kazi Cha 18 Cha Maafisa Habari na Mawasiliano wa Serikali Dar es Salaam,2023


TCRA Kushiriki Kikao Kazi Cha 18 Cha Maafisa Habari na Mawas...

 

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano kwa Umma wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Bi. Lucy Mbogoro atatoa wasilisho kuhusu mfumo wa Leseni za Mawasiliano na namna ya kuomba leseni kupitia 'Tanzanite Portal.'      Wasilisho litatolewa siku ya  Jumanne, tarehe 28 Machi 2023 katika Kikao cha 18 cha Maafisa Habari na Mawasiliano wa Serikali (TAGCO) katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Julius Nyerere, Dar es salaam.

Maafisa habari wote wa Serikali ambao wangependa kuanzisha Kituo cha Utangazaji wa Redio au Televisheni-mtandao (Online TV) wanahimizwa kushiriki ili kupata elimu ya utaratibu wa kuomba Leseni za Maudhui ya Utangazaji kupitia mfumo wa Tanzanite.

Je, una Maswali yoyote juu ya Sekta ya Mawasiliano?
Tuma Mrejesho na Malalamiko!

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imejidhatiti kutoa huduma bora kwa wateja na wadau wake wote.

Tuma Mrejesho na Malalamiko!